KAMPUNI YA KUUZA VIRUTUBISHI YA GREEN WORLD

Unatafuta Biashara Ya Mtaji Mdogo?

Leo napenda tuizungumzie kampuni ya kuuza virutubishi ya Geen World yenye ofisi zake mjini Dar Es Salaam. Katika ukurasa huu nitatoa maelezo kidogo kuhusu shughuli za kampuni hii, aina ya virutubishi ambavyo huuzwa na kampuni hii na jinsi ambavyo wewe mtanzania unavyoweza kunufaika kwa kujiunga na kampuni hii na  kufanya biashara ambayo itakubadishia maisha yako kwa mtaji mdogo sana.

Nimeona ni lazima niizungumzie kampuni hii kwa sababu watanzania wengi tayari wamenufaika sana kupitia kampuni hii, wengi wao wanapata vipato vikubwa sana kwa mwezi na wengine wamefikia kupewa magari yenye thamani ya hadi shilingi milioni ishirini.

Watu ninaowazungumzia si watu wenye elimu kubwa au waliokuwa na mitaji mikubwa sana, la hasha, ni watanzania wa kawaida tu waliokuwa na ari ya kufanya biashara na walipoisikia kampuni hii walijiunga mara moja na kujituma ipasavyo.

Endelea kusoma ili uijue kampuni hii.

Ijue Kampuni Ya Green world

Green World USA ni kikundi cha makampuni ya kimataifa kinachoshughulika na utafiti wa kisayansi, uendelezaji na uzalishaji wa madawa ikiwa ni pamoja na dawa zinatozotokana na mimea na vipodozi, kikiwa na makao yake makuu katika mji wa Michigan nchini Marekani na viwanda vyake vya uzalishaji huko South Carolina (Marekani), Nanjing na Tianjin (China).

 

Prof Deming Li

Muasisi wa kampuni hii Dk. Deming Li alikuwa na dhamira moja kuu ya kutumia mimea na hasa mimea ya asili ya China na matokeo ya tafiti zake binafsi alizozifanya kupata hazina ya bidhaa zitakazomsaidia kila mtu popote pale alipo katika dunia yetu.

virutubisho vya Green World

Kampuni ya Green World iliundwa kutengeneza bidhaa zinazotokana na mimea na vitu vya asili kwa kutumia utaalamu wa hali ya juu wa kisasa. Kwa kushirikiana na vituo vya utafiti na vyuo vikuu mbalimbali, kikiwepo chuo kikuu cha Cornell (USA), kampuni hii imeweza kutengeneza bidhaa mbalimbali za tiba-lishe, bidhaa ambazo hadi sasa zimeleta na kutoa mchango mkubwa katika kuboresha afya ya binadamu.

Bidhaa za kampuni hii zimepokelewa na zinatumika sana katika nchi za China, Marekani na nchi za kusini mashariki mwa bara la Asia hasa Indonesia.

Bidhaa Za Kampuni Ya Green World

Kampuni ya Green World USA hadi sasa imefanikiwa kutengeneza virutubishi vya asili vya aina tofauti (zaidi ya aina mia moja) ambavyo husambazwa katika nchi zaidi ya 90 duniani. Tunaweza kwa haraka haraka kuvigawanya virutubishi hivi au dawa hizi katika makundi kutokana na tatizo linalohusika. Green World wanazalisha virutubishi au dawa kwa ajili ya matatizo yafuatayo:

1.  Matatizo Ya Mifupa Na Viungio Vya Mifupa
2.  Matatizo Ya Maambukizi Ya Wadudu
3.  Matatizo Ya Kuwa Na Uzito Mkubwa (Unene).
4.  Matatizo Ya Ubongo
5.  Magonjwa Ya Watoto
6.  Magonjwa Na Afya Ya Akina Mama
7.  Matatizo Na Afya Ya Mwanamme
8.  Afya Ya Macho
9.  Matatizo Ya Uyeyushaji Chakula Tumboni
10. Matatizo Ya Ngozi
11. Ukosefu Wa Kinga Ya Mwili
12. Matatizo Ya Moyo
13. Kansa

Jinsi Ya Kufanya Biashara Kwa Mtaji Mdogo Kabisa Na Kampuni Hii

Kufanya biashara na kampuni hii ni rahisi sana, unachotakiwa biashara kwa manesikukifanya ni kujiunga kwa TZS 35,000/ tu. Ukishajiunga kwa kiasi hicho cha pesa utapewa kitambulisho cha kampuni na kifurushi cha kuanzia chenye maelezo muhimu na utatakiwa kuhudhuria mafunzo ya bure ya jinsi ya kuendesha biashara hii. Baada ya hapo utatakiwa kuwaeleza ndugu, rafiki na watu wengine kuhusu uwepo wa virutubishi hivi na jinsi wanavyoweza kuweka afya zao katika hali nzuri au kujiponya na magonjwa nyemelezi.  Wewe utauziwa virutubishi kwa bei ya jumla kama msambazaji wa kampuni na utaziuza kwa faida utakayoiweka mfukoni mwako.

Baadaye, utalipwa bonasi ya asilimia ishirini ya thamani ya mauzo uliyoyafanya katika mwezi.

Ili uweze kupata kipato kikubwa zaidi, utawajibika kuwashauri ndugu na rafiki wengine kujiunga na biashara hii, hapo ndipo utakapokuwa umeanza kujenga timu yako. Na sasa utaanza kupata malipo ya ziada ambayo yatatokana na mauzo ya watu wa timu yako. Malipo ya ziada utakayopata kwa mwezi yatalingana na ukubwa wa timu uliyoijenga chini yako. Rahisi kabisa!

Biashara hii  hufanywa kwa njia ya mawasiliano ya mdomo (word of mouth) hivyo inamfaa mtu yeyote, ni biashara kwa akina mama wa nyumbani, ni biashara kwa mwanafunzi chuoni, ni biashara kwa mfanyakazi katika ofisi, biashara kwa mwalimu wa shule, biashara bora kwa nesi katika hospitali…  ni biashara ya mtaji mdogo kwa mtu yeyote! Ili kuona kwa nini biashara hii ni bora kwa jamii ya watu wetu wa Tanzania, soma ukurasa wa “Ubora Wa Kampuni Ya Green world Tanzania“.

Wapo walionufaika na wanaolipwa pesa nyingi kwa mwezi katika kila kundi nililolitaja hapo juu. Usiogope kwamba utashindwa kujenga timu yako kwa sababu utapewa mafunzo na msaada kutoka kwa mtu aliyekushauri kujiunga na biashara hii na utaweza tu.

Pichani hapo juu ni baadhi ya wanachama wa barani Afrika waliofanya vizuri katika biashara hii wakapewa tuzo mbalimbali ikiwa ni pamoja na magari na fursa za kutembelea nchi mablimbali za dunia kwa gharama ya kampuni.

Soma moja ya shuhuda za wanachama wa kampuni ya Green world hapa chini:

 

USHUHUDA WANGU WA KAMPUNI YA GREEN WORLD

Naitwa Hilda Mahende, naishi Tabata Segerea (Kwa Bibi) mjini Dar Es Salaam. Kabla ya kuanza kufanya biashara za mtandao nilikuwa nauza duka la madawa hapa hapa mjini Dar Es Salaam. Siku moja katika kutafuta dawa za kumtibu mgonjwa wangu nilikutana na kijana mmoja ambaye alinieleza ubora wa kutumia dawa za kampuni ya Green World. Baada ya kununua dawa hizo na mgonjwa wangu kupona, nilikwenda kumshukuru kaka huyo na katika maongezi alinishawishi nijiunge na kampuni hiyo.

ushuhuda wa Hilda wa kampuni ya Green World

Niliamua kujaribu na kujiunga nayo mwezi March 2013. Nilifanya kazi ya kuuza dawa kidogo kidogo na katika mwezi huo huo wa kwanza nilifanikwa kuuza dawa za thamani ya Tshs 400,000/, wakati huo huo nilikuwa nikiwapa taarifa na kuwashawishi marafiki zangu kujiunga na kampuni hii. Hadi Oktoba 2013 nilikuwa nimefika ngazi ya 6*C na nikapewa fursa ya kutembelea miji ya Nianjin, Hanzou, Suanzou na Shanghai huko Uchina kwa gharama za kampuni.

Baada ya hapo nilipata kishawishi cha kujiunga na kampuni nyingine na kuiacha Green World nikifikiri kwamba ningepata mafanikio zaidi kwenye hiyo kampuni niliyoambiwa. Baada ya kuona hiyo haikuwa nzuri, nilitafuta nyingine. Niliyumba na kujiunga na kampuni nyingi tu, moja baada ya nyingine bila kupata mafanikio makubwa kama nilivyotegemea.

Nakumbuka siku moja nilikutana na kaka anayeitwa  Jerome, nilimsimulia kuhusu ninavyokosa maendeleo kutoka kwenye biashara za mtandao. Baada ya kunisikiliza kwa makini, Jerome aliniambia kuwa lilikuwa kosa kubwa sana kuiacha kampuni ya Green World. Akanifafanulia makosa yote niliyokuwa nimeyafanya wakati nikifanya biashara ya kampuni hiyo, kisha akanipa mwongozo wa jinsi ya kufanikiwa na Green World. Kwa vile niliona waziwazi makosa yangu na ukweli katika maneno yake, niliamua kurudi upya na nguvu mpya kwenye kampuni yangu ya zamani. Hiyo ilikuwa Aprili 2014.

Niliamua kuanza upya kabisa na kufuata mwongozo wa kaka Jerome. Hivi leo ninavyoandika ushuhuda huu (Februari 2015) nimefikia ngazi ya 7*C na ninapata bonus ya zaidi $1000 kwa mwezi na nafurahi kukuambia msomaji wangu kwamba tarehe 28 Februari 2015 nimekuwa mmoja kati ya wanachama wanne tuliopewa magari yenye thamani ya Tshs milioni 18 kila moja kama tuzo kwa kazi yangu ya miezi 10 tu, kwenye sherehe iliyofanyika katika ukumbi wa Blue Pearl Hotel (Ubungo Plaza).

 

zawdi ya gari Hilda Green World

 

Natoa ushuhuda huu kwamba biashara za mtandao ni za kweli, kinachotakiwa kwanza ni kuchagua vizuri kampuni ya kufanya nayo kazi. Pili ni kusoma kwa makini na kuelewa mpangilio wa kampuni yako. Tatu na mwisho ni kujituma katika kampuni yako bila kuyumbayumba toka kampuni moja hadi nyingine. Kwangu mimi, Green World ndiyo kampuni bora ya mtandao nchini Tanzania.

Karibu Green World, nipo tayari kukuongoza kwa lo lote ili uweze kupata mafanikio makubwa hata zaidi ya haya niliyopata mimi.

Ahsante kwa kusoma ushuhuda wangu. Nakukaribisha Green World kwa mikono miwili.

Umependa Kujiunga Na Kampuni Ya Green World?

 

Kampuni ya Green World ni fursa ya kimaajabu sana kwani inamwezesha mtu  ye yote kupata maisha ya ndoto zake katika muda mfupi bila kujali elimu au mtaji alio nao. Lakini, ieleweke toka mwanzo kabisa kuwa kampuni haigawi pesa, bali inakupa fursa na masomo ili juhudi zako binafsi zikubadilishe wewe mwenyewe – utatakiwa kujifunza na kujituma. Hivyo, basi kabla ya kujiunga moja kwa moja, jipime kwa kuusoma ukurasa huu, na kisha chini yake utapata fursa ya kuungana na Green World.

Bofya juu ya maandishi yafuatayo: Kabla ya kujiunga na kampuni ya Green World.

Kwa mawasiliano tuma ujumbe wako kupitia ukurasa huu kwa kujaza fomu hapa chini , au tuma barua pepe kwa anuani promota927@gmail.com au piga simu ndani ya muda wa kazi kwenye nambari zifuatazo: 0655 858027 au 0756 181651.

Tafadhali tembelea blog yetu kujisomea mada mbali mbali zinazohusu biashara za mtandao na fursa za kufanya biashara za mtandao. Humo unaweza kuona wasomaji wengine wana maoni gani kuhusu mada zetu tunazoziandika. Pia unakaribishwa kuona video mbali mabali zinazohusu biashara ya mtandao ya kampuni ya Green World kwenye channel yetu ya YouTube.

Kutembelea blog bofya HAPA.
Kutembelea channel yetu ya YouTube bofya HAPA.